Zaburi124swh_onmm
Shukrani kwa ukombozi wa Israeli
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
1Kama Mwenyezi Mungu hangekuwa upande wetu;Israeli na aseme sasa:2kama Mwenyezi Mungu hangekuwa upande wetu,watu walipotushambulia,3hasira yao ilipowaka dhidi yetu,wangetumeza tukiwa hai,4mafuriko yangegharikisha,maji mengi yangetufunika,5maji yaendayo kasiyangetuchukua.6Ahimidiwe Mwenyezi Mungu,ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.7Tumeponyoka kama ndegekutoka mtego wa mwindaji;mtego umevunjika,nasi tumeokoka.8Msaada wetu ni katika jina la Mwenyezi Mungu,Muumba wa mbingu na dunia.