1Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako,ikiwa umeshikana mikono kwa kuweka ahadikwa ajili ya mwingine,2kama umetegwa na ulichosema,umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,3basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru,kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako:Nenda ukajinyenyekeshe kwake;msihi jirani yako!4Usiruhusu usingizi machoni pako,usiruhusu kope zako zisinzie.5Jiweke huru, kama paa kutoka mkononi mwa mwindaji,kama ndege kutoka mtego wa mwindaji.6Ewe mvivu, mwendee mchwa;zitafakari njia zake ukapate hekima!7Kwa maana yeye hana msimamizi,wala mwangalizi, au mtawala,8lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazina hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.9Ewe mvivu, utalala hata lini?Utaamka lini kutoka usingizi wako?10Kulala kidogo, kusinzia kidogo,kukunja mikono kidogo upate kupumzika:11umaskini utakuja juu yako kama mnyang’anyi,na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.12Mtu mbaya sana na mlaghai,ambaye huzungukazungukana maneno ya upotovu,13ambaye anakonyeza kwa jicho lake,anayetoa ishara kwa miguu yakena kuashiria kwa vidole vyake,14ambaye hupanga ubayakwa udanganyifu moyoni mwake:daima huchochea fitina.15Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula;ataangamizwa mara moja, pasipo msaada.16Kuna vitu sita anavyovichukia Mwenyezi Mungu, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:17macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,18moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,19shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
Onyo dhidi ya uasherati
20Mwanangu, zishike amri za baba yako,wala usiyaache mafundisho ya mama yako.21Yafunge katika moyo wako daima,yakaze kuizunguka shingo yako.22Unapotembea, yatakuongoza;unapolala, yatakulinda;unapoamka, yatazungumza nawe.23Kwa maana amri hii ni taa,mafundisho haya ni mwanga,na maonyo ya nidhamuni njia ya uzima,24yakikulinda na mwanamke aliyepotoka,kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.25Moyo wako usitamani uzuri wake,wala macho yake yasikuteke,26kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini,hata ukose kipande cha mkate,naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.27Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lakebila nguo zake kuungua?28Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya motobila miguu yake kuungua?29Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine;hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.30Watu hawamdharau mwizi akiibaili kukidhi njaa yake akiwa na njaa.31Lakini akikamatwa, lazima alipe mara saba,ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.32Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa;yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.33Mapigo na aibu ni fungu lakena aibu yake haitafutika kamwe;34kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume,naye hataonesha huruma alipizapo kisasi.35Hatakubali fidia yoyote;atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.