Mithali1swh_onmm
1Mithali za Sulemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:2Kwa kupata hekima na nidhamu;kwa kufahamu maneno ya busara;3kwa kujipatia nidhamu na busara,kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;4huwapa busara wajinga ,maarifa na akili kwa vijana;5wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao,wenye kupambanua na wapate mwongozo;6kwa kufahamu mithali na mifano,misemo na vitendawili vya wenye hekima.7Kumcha Mwenyezi Mungu ni chanzo cha maarifa,lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.