Amosi2swh_onmm
1Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu:“Kwa dhambi tatu za Moabu,hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu.Kwa sababu alichoma mifupa ya mfalme wa Edomu,ikawa kama chokaa.2Nitatuma moto juu ya Moabuambao utateketeza ngome za Keriothi.Moabu ataanguka kwa ghasia kubwakatikati ya kelele za vita, na sauti ya tarumbeta.3Nitamwangamiza mtawala wakena kuwaua maafisa wake wote pamoja naye,”asema Mwenyezi Mungu.4Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu:“Kwa dhambi tatu za Yuda,hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu.Kwa sababu wameikataa Torati ya Mwenyezi Munguna hawakuzishika amri zake,kwa sababu wamepotoshwa na miungu ya uongo,miungu ambayo babu zao waliifuata.5Nitatuma moto juu ya Yudaambao utateketeza ngome za Yerusalemu.”